Blogroll
Jumatatu
Mgeni rasmi Mkurugenzi msaidizi Wizara ya Sayansi na Teknolojia idara ya sayansi na ubunifu Dr. Magreth Komba akizindua kijarida cha WITTED kuashiri uzinduzi wa mpango wa kuhamasisha wanawake kusomea uhandisi sayanzi na teknolojia.
Mgeni rasmi Mkurugenzi msaidizi Wizara ya Sayansi na Teknolojia idara ya sayansi na ubunifu
Dr. Magreth Komba
Picha ya pamoja
Posted on 04:21 by Unknown

Ufumbuzi riwaya imekuwa kupatikana kwa matatizo, ambayo ni pamoja na polisi kupokea rushwa, makosa ya usalama barabarani na masaa katika foleni .
Robots ni kushikamana na kompyuta kuu , na wamejenga katika kamera , ambayo ripoti ya makosa ya usalama barabarani katika muda halisi. Hii hupunguza hatari ya shughuli yoyote ya kukwepa, kama vile rushwa. Ukosefu wa binadamu hufanya kutekeleza sheria rahisi.Wao ni umbo kama polisi trafiki binadamu, na taa za barabarani nyuma yao na kifua .
Haja ya robots haya uliojitokeza kwa sababu madereva na watembea kwa miguu sawa walilalamika kuhusu shughuli ya kukwepa, na uvivu wa maafisa wa usalama barabarani.
Posted on 03:21 by Unknown
Jumamosi
ENGLAND KWA `PAMBA` HAWAKAMATI, CHEKI SUTI NA MOKA WATAKAZOTUPIA KUELEKEA KOMBE LA DUNIA BRAZIL 2014

Pamba
zinavutia?: Wachezaji wa timu ya Taifa ya England (kutoka kushoto
kwenda kulia) Andros Townsend, Adam Lallana, Jermain Defoe, Leighton
Baines, Steven Gerrard, Ashley Cole, Frank Lampard, Chris Smalling,
Michael Carrick, Gary Cahill, John Ruddy na Rickie Lambert wakionesha
suti zilizobuniwa na Marks na Spencer kwa ajili ya kombe la duniani
mwaka huu nchini Brazil.
England kwa kupendeza ni kiboko yao.

Wametokelezea
bomba: Nyota wa simba watatu (kutoka kushoto kwenda kulia) Leighton
Baines, Frank Lampard, Steven Gerrard na Ashley Cole wanatarajiwa kuvaa
suti mpya wakielekea Brazil kushiriki kombe la dunia

Zimepimwa vizuri: Kila mchezaji wa kikosi cha Roy Hodgson atavaa suti ya Marks na Spencer


Kombe
lililopita: Bosi wa wakati huo wa England, Fabio Capello akiwa na
kikosi chake kilichovalia suti za Marks na Spencer mwaka 2010 wakati wa
kombe la dunia nchini Afrika kusini
Posted on 00:39 by Unknown

Afisa
Mipango Kitengo cha Mawasiliano, Habari na Tehama UNESCO, Bw. Al Amin
Yusuph, akiwasilisha mada kuhusu mchango wa uhuru wa vyombo vya habari
katika utawala bora, kukuza uwezo na kupunguza umaskini kongamano la
waandishi wa habari lilioandaliwa kama sehemu ya maadhimisho ya siku ya
Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yanayofanyika jijini Arusha.
“Kwa
sasa tasnia hii iko kwenye wakati mgumu sana kwani hata marais wa nchi
mbalimbali mfano Uganda, Kenya hata Marekani wanakinzana na vyombo vya
habari kwa madai kuwa kauli zao zinapotoshwa, laikini ukweli ni kwamba
ni vyema kauli hizo za viongozi zikachunguzwa kwa undani zaidi ili
kuelewa iwapo zina uwajibikaji ndani yake,” alisema Kibanda.
Kibanda
aliongeza kuwa wakati umefika sasa kwa waandishi kutambua kuwa kuna
ajenda za siri zilizojificha dhidi ya uteswaji wa waandhishi wa habari
hivyo yasidharauliwe, yafanyiwe kazi kwa kina ili kuelewa kiini cha
tatizo kwa kupata ufumbuzi.
Kwa
upande wake mwandishi mkongwe na aliyetunukiwa tuzo ya maisha mwaka
2012 na Baraza la Habari Hamza Kasongo alisema vyombo vya habari vina
nguvu kubwa katika kushawishi hivyo vitumie nguvu hiyo kama muhimili wa
nne wa nchi katika kuzikabili changamoto zilizopo.
“Kuwe
na mtandao unaoeleweka wa mawasaliano kati ya waandishi wa habari
nchini ili kuhakikisha kuwa matatizo yaliyopo yanatatuliwa bila woga na
kwa ujasiri kwa lengo la kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa,” alisema
Kasongo.
Posted on 00:20 by Unknown

Wakati mvua kubwa zimenyesha Dar es salaam siku kadhaa zilizopita baadhi ya watu waliilalamikia Serikali kwamba imefanya uzembe manake kama ingekua imejenga miundombinu vizuri, maeneo ambayo yangekumbwa na maafuriko ni machache.
Post hii ni maalum kwa ajili ya hiki kilichotokea kwenye jiji la Baltimore Marekani ambapo mvua kubwa imesabisha kuzama kwa mtaa uliokua umejengwa vizuri kabisa lakini umemezwa na magari yaliyokua yamepaki juu yake.


Posted on 00:14 by Unknown

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda akiwaasa wabunge wote kushiriki kikamilifu katika kamati zao kizalendo kwa kujali nchi yao ili ipatikane bajeti yenye tija kwa taifa leo (jana) wakati wa kupokea taarifa ya Wizara ya fedha jijini Dar es salaam.

Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum akiwasilisha taarifa ya sura ya Bajeti kuu ya Serikali kwa wabunge leo (jana) jijini Dar es salaam inayotarajia kuanza kutumika kwa mwaka wa fedha unaoanza Julai 2014/2015.

Posted on 00:11 by Unknown
Ijumaa

Ni rasmi kwamba Clouds Media International imepewa leseni ya kurusha matangazo katika nchi za umoja wa falme za kiarabu (UAE) ambapo mkurugenzi Mtendaji Joseph Kusaga amesema sasa kituo cha Clouds TV kimataifa kitakuwa kikishuhudiwa na watu wa mataifa mbalimbali.
Clouds TV kimataifa ni mwendelezo wa televisheni maarufu sana kwa vijana nchini Tanzania, hata hivyo sehemu kubwa ya maudhui yatakayokuwemo kwenye Clouds TV kimataifa itakuwa na mpangilio mpana wa vipindi kwa watazamaji vitakavyorushwa kwa lugha za Kiingereza na Kifaransa.
Akieleza zaidi Kusaga amesema “Leo ni siku ya kihistoria na alama ya hatua moja katika mpango wetu wa kina wa kupeleka maudhui ya Clouds TV kimataifa kupitia matangazo kwa njia ya mitandao’’.

Clouds TV kimataifa haitotoa tu burudani lakini pia itakuwa kiunganishi kwa waafrika waishio katika umoja wa nchi za falme za kiarabu pamoja na kuwapa fursa za kutangaza bidhaa zao na kuimarisha uhusiano baina yao.
Vituo vya televisheni katika Umoja wa falme za kiarabu vipo vingi na vyenye ushindani mkubwa, lakini Clouds TV kimataifa imebahatika kupata nafasi ya kurusha matangazo yatakayowafikia walengwa katika chaneli yenye uwezo wa kuwahudumia zaidi ya watazamaji takribani milioni 3.5 kutoka katika nchi za Afrika. Kwa sasa hakuna kituo kinachotoa huduma hii na hivyo kuwa fursa muhimu kwa watazamaji.
Clouds TV kimataifa itarusha vipindi vya burudani, tamthilia, maigizo, ucheshi, na muziki, vyote vitakavyo kuwa vimeandaliwa kutoka nchi za mashariki, magharibi na kusini mwa bara la afrika na itapatikana kwa watazamaji walio katika Umoja wa falme za kiarabu kupitia huduma ya IPTV inayotolewa na Etisalat na Du.
Clouds TV kimataifa itarushwa kupitia mamlaka ya Abu Dhabi ijulikanayo kama twofour54, ikiungana na vituo kama FOX na CNN.
Clouds TV kimataifa itaanza kurusha matangazo ya majaribio katika wiki chache zijazo kabla ya tarehe 15 mwezi June mwaka huu.
Posted on 07:36 by Unknown

Mpaka sasa video hii imetazamwa zaidi ya mara laki moja na elfu 30 kwenye mtandao wa Youtube toka ianze kuonyeshwa April 29 2014 ikiwa ni video ya kipekee na ya kiwango kingine cha juu tofauti na ilivyozoeleka kwa Sauti Sol.
Mtandao wa Kenya ghafla.co.ke umeripoti kwamba imefahamika video hii imezuiwa kuchezwa kwenye TV stations mbalimbali za Kenya kwa sababu imevunja maadili.
Kwenye Mdundo Awards jana usiku Bien Aime wa Sauti Sol alisema mwanasheria wao anashughulikia ishu ya kufungiwa kwa video yao ambayo imeambiwa inachochea ngono kutokana na uwazi wa wanaookenana ndani yake.
Hii itakua video nyingine iliyochukua headlines zinazofanana na ile ya P Unit ‘you guy’ ambayo ilifungiwa na CITIZEN TV kwa sababu ya mrembo alieliachia umbo lake kwa sana.
Posted on 07:34 by Unknown

Usiku wa kuamkia leo Maafisa nchini Nigeria wametoa taarifa kuhusu mlipuko uliotokea na kuua watu 19 katika kituo cha basi katika mji mkuu wa taifa hilo Abuja.
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa idara ya kushughulikia mikasa na hali ya dharura- FEMA- Abbas G Idriss, watu 60 walijeruhiwa vibaya lakini 6 kati yao wametibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani pia magari sita yameharibiwa katika mlipuko huo.
Mlipuko huo umetokea katika eneo la Nyanya ambao uko karibu na kituo cha basi ambako zaidi ya watu sabini waliuwawa katika shambulizi la tarehe14 mwezi Aprili.

Ripoti za awali zimesema kuwa watu kadhaa wameuwawa na wengine wengi kujeruhiwa,Waandishi wanasema kuwa mlipuko huo umesababishwa na bomu lililotegwa ndani ya gari,Mmoja wa walioshuhudia kisa hicho amesema aliona miili 20 ya watu waliouwawa.
Mpaka sasa hakuna kundi lililodai kuhusika katika shambulizi hilo lakini kundi la wanamgambo wa kiislamu la Boko Haram limewahi kutekeleza mashambulizi kama hayo mjini Abuja,Mengi ya mashambulizi ya Boko Haram yamekuwa yakitokea katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Bomu la tarehe 14 Aprili lilizua hofu kwamba huenda wanamgambo hao wameanza kupanua maeneo wanayoendeleza harakati zao.
Posted on 07:32 by Unknown

Kumbe hata Marekani kuna wanaohukumiwa kunyongwa kimakosa?

Uchunguzi mpya uliofanywa nchini Marekani unaonyesha mmoja kati ya wafungwa 25 wa mauaji hakufanya kosa hilo hivyo zaidi ya asilimia 4 kati ya wafungwa wa kimarekani wamehukumiwa kifo lakini hawakutenda makosa hayo.
Wachunguzi kutoka Pennsylvania, Michigan na kwengineko wamekaa pamoja kuchunguza kitu kinachoitwa “Dark figure” yaani hesabu ya wafungwa waliohukumiwa kifo na wakati hawakufanya uhalifu unaowafanya wahukumiwe kifo.
Matokeo ya uchunguzi huo ambayo yalichapishwa na (National Academy of Science of the United States) yameonesha kuwa mauaji ya watu wasio na hatia yamekua kitu cha kawaida nchini humo.

Walionyongwa/kuuliwa bila ya hatia wamezidi kutoka asilimia 1.6 mpaka asilimia 4.1 ambapo wafungwa 340 walikuwa wawe wameshatolewa ndani ya miaka 30 iliyopita na 138 kati yao walinusurika na adhabu hiyo.
Wengi walinusurika na adhabu hiyo kati ya miaka ya 1993 mpaka 2004 ambapo watu 2,675 walitolewa katika orodha ya kuuliwa baada ya uangalizi wa makini kufanyika tena katika kesi zao ambapo hiyo ni asilimia 36 ya watu waliokutwa na adhabu hii kati ya miaka hiyo.
Hata hivyo hawakuachiwa huru pamoja na kwamba waliondolewa adhabu ya kunyongwa badala yake walipewa adhabu nyingine na wengi wao wakihukumiwa kifungo cha maisha.
Posted on 07:29 by Unknown

Kikosi cha United msimu uliopita.
Wakati David Moyes alipoambiwa kuwa ameteuliwa rasmi kuwa kocha wa
Manchester United baada ya Sir Alex Fergusson alikuwa na uhakika kuwa
maisha yake kama kocha yatabadilika kwa kiasi fulani . Moja ya mazingira
magumu aliyokuwa akikutana nayo akiwa Everton ni ufinyu wa bajeti
ambayo ilikuwa inamfanya awe kwenye wakati mgumu kujaribu kupata
wachezaji kwa bei za bure .Moyes alidhani kuwa tatizo hilo linaweza kuwepo United na alishangaa alipoambiwa kuwa fedha si tatizo Man United tatizo ni yeye tu . Hiyo ndio kauli iliyotoka kwa wamiliki wa Manchester United ambao ni familia ya Glazer inayoongozwa na mzee Malcolm Glazer akisaidiwa na wanae Joe na Avram Glazer ambao wamesema kuwa wako tayari kumletea David Moyes Jembe lolote analotaka kulisajili ili mradi tu awe kwenye mazingira mazuri kwenye msimu wake wa kwanza.
David Moyes ambaye jana aliiongoza United katika mchezo wake wa kwanza ambao timu hiyo ilifungwa 1-0 na Thai All Stars amekuwa akiwasaka wachezaji kadhaa kimya kimya na kumekuwa na tetesi ambazo zimeihusisha United na wachezaji kama Gareth Bale , Cristiano Ronaldo na Thiago Alcantarra.
Hata hivyo hadi sasa United imepeleka ofa moja tu ya kumsajili beki wa kushoto Leighton Baines ya paundi milini 12 ambayo hata hivyo klabu ya Everton imeikataa. United wanaelekea kumkosa kiungo ambaye walitajwa kuwa mbioni kumsajili ambaye ni Thiago Alcantarra aliye karibu kukamilisha usajili kwenda Bayern Munich.
Posted on 07:23 by Unknown

Naona hii ni historia kabisa aisee….. yani Rais Jakaya Kikwete anaweza hata kuingizwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za dunia kwa kukubali mwaliko wa kuwa refa na kuchezesha mechi ya Wabunge wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania wa timu za Simba na Yanga jumapili July 7 2013.
Taarifa ambayo nimepewa na Global Publishers ambao ndio waandaaji, ni kwamba Rais amekubali kuwa refa kwenye Tamasha la Matumaini litakalofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam ambalo sehemu ya mapato yake yatasaidia elimu Tanzania.
Ni mara ngapi tunamuona President wetu kwenye sehemu rasmirasmi akiwa mgeni rasmi? ni mara ngapi tunatamani kuona upande wake wa pili kwenye ishu kama hizi? basi Jumapili hii itakua burudani na pia vichekesho… yani ukijaribu kutengeneza picha President na umri wake, na umbo lake, na cheo chake alafu apulize filimbi?????
Yani anakuwa refa na jezi zake kabisa…. na tumeshamzoea siku zote huwa anatokelezea hivi yani….


Posted on 07:20 by Unknown
NMB kwa kupitia idara yake ya biashara za Kilimo (Agribusiness Department) imetoa ripoti mbili;
1.Utafiti
wa kujua kama mfumo wa stakabadhi mazao ghalani (Warehouse Receipt
Financing Sytem) una manufaa kwa wakulima au la? Utafiti umethibitisha
kuwa mfumo una manufaa kwa wakulima japokuwa kuna changamoto bado, mfano
wakulima wa kahawa wanaouza mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi
ghalani wanapata zaidi ya asilimia 30% ukilinganisha na wale wasiotumia
mfumo wa stakabadhi ghalani.
2. Utafiti
wa sekta ya sukari unaonesha kuwa Tanzania inatumia wastani wa tani
520,000 kwa mwaka (ikiwemo sukari kwa matumizi ya viwanda) kati ya hizo
uzalishaji ni tani 300,000 na kiasi cha tani 220,000 zinaingizwa kutoka
nje kwa mwaka, utafiti pia umeonyesha kwamba Tanzania inaweza kuzalisha
kiwango cha kutosheleza mahitaji ya nchi iwapo kutakuwa na kilimo cha
umwagiliaji, miche bora ya miwa, pembejeo za kilimo zilizo bora ikiwemo
mbolea pamoja na mazingira bora ya uwezeshaji (enabling environment) wa
sekta ya sukari.

NMB wanaoshiriki maonesho ya Sabasaba yanayoendelea

Maofisa
wa NMB Idara ya biashara ya Kilimo, kwanza kulia ni Sierk Plaat ambae
ni Mchambuzi Mwandamizi toka benki ya Rabobank, Robert Paschal Mkuu wa
Idara Mikopo ya Kilimo NMB na Carol Nyangaro Mtafiti, Mchambuzi wa
mambo ya kilimo wakionyesha kitabu ambacho kimebeba ripoti ya mfumo wa
stakabadhi ghalani.

Mkuu wa Idara ya biashara za kilimo NMB, Robert Paschal (kati) akiongea na waandishi wa habari na kuwasilisha ripoti ya biashara za kilimo zifanywazo na Benki ya NMB
Posted on 07:17 by Unknown
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)
Tz

Popular Posts
-
Siku chache baada ya taarifa za kutoka Morogoro zilizomhusu Mtoto Nasra ambaye kwa sasa ni marehemu ambaye alifungiwa kwenye box kwa miak...
-
Bunge la bajeti linaendelea bungeni mjini Dodoma ambapo sasa ni zamu ya wizara ya fedha na uchumi. Bajeti yake imewasilishwa na waziri w...
-
Tupo kwenye ukumbi AICC arusha kwenye kongamano la vyombo vya habari. Ikiwa ni siku ya uhuru wa vyombo vya habari
-
*KUELEKEA KUMBUKUMBU YA 'KARUME DAY' TUJIKUMBUSHE NA KILE KILICHOTOKEA KUPEKEA KIFO CHAKE Miaka 42 iliyopita, Aprili 7, 1972; Rai...
-
Mambo yanaendelea kuiva taratibu tayari kuelekea Brazil from 12 June to 13 July 2014. Hiyo itakuwa mara ya pili kwa Brazil kuandaa Faina...
-
Chatu akiwa anatamba pembeni ya ukuta kuingia ndani ya nyumba Chatu akiwa ndani ya eneo la hiyo nyumba Hii imetokea Mkoani Aru...
-
Ni rasmi kwamba Clouds Media International imepewa leseni ya kurusha matangazo katika nchi za umoja wa falme za kiarabu (UAE) ambapo m...
-
Home » General News » Kumbe hata Marekani kuna wanaohukumiwa kunyongwa kimakosa? Kumbe hata Marekani kuna wanaoh...
Recent Post
Blog Archive
-
▼
2014
(39)
-
▼
Mei
(17)
- WANAWAKE KUSOMEA FANI YA UHANDISI SAYANSI NA TEKNO...
- Nagging majeraha kudhoofisha wachezaji muhimu VPL
- Congo kuweka Robots Trafiki
- ENGLAND KWA `PAMBA` HAWAKAMATI, CHEKI SUTI NA MOKA...
- MEZA YA MAGAZETI LEO JUMAMOSI
- UHURU WA VYOMBO VYA HABARI
- WAANDISHI WA HABARI MSIKUBALI KUTUMIWA, UNGANENI
- Kama ulidhani mvua ni mbaya Dar tu, hii ni Marekan...
- BAJETI KUU YA SERIKALI: takribani Sh. Tril. 19. 7 ...
- Good news ya Clouds TV ya kimataifa, kituo cha kwa...
- Ni zamu ya Kenya tena, hii ndio nyingine mpya iliy...
- Home » General News » Kuhusu mlipuko uliotokea usi...
- Kumbe hata Marekani kuna wanaohukumiwa kunyongwa k...
- David Moyes aambiwa kuwa fedha si shida United
- Ujumbe wa Akon kwa kila Muamerika mweusi anaeishi ...
- Umezisikia taarifa za Rais Kikwete kuwa refa wa Si...
- NMB: Mnawarahisishia mpaka wakulima
-
▼
Mei
(17)
Inaendeshwa na Blogger.