
Afisa
Mipango Kitengo cha Mawasiliano, Habari na Tehama UNESCO, Bw. Al Amin
Yusuph, akiwasilisha mada kuhusu mchango wa uhuru wa vyombo vya habari
katika utawala bora, kukuza uwezo na kupunguza umaskini kongamano la
waandishi wa habari lilioandaliwa kama sehemu ya maadhimisho ya siku ya
Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yanayofanyika jijini Arusha.
“Kwa
sasa tasnia hii iko kwenye wakati mgumu sana kwani hata marais wa nchi
mbalimbali mfano Uganda, Kenya hata Marekani wanakinzana na vyombo vya
habari kwa madai kuwa kauli zao zinapotoshwa, laikini ukweli ni kwamba
ni vyema kauli hizo za viongozi zikachunguzwa kwa undani zaidi ili
kuelewa iwapo zina uwajibikaji ndani yake,” alisema Kibanda.
Kibanda
aliongeza kuwa wakati umefika sasa kwa waandishi kutambua kuwa kuna
ajenda za siri zilizojificha dhidi ya uteswaji wa waandhishi wa habari
hivyo yasidharauliwe, yafanyiwe kazi kwa kina ili kuelewa kiini cha
tatizo kwa kupata ufumbuzi.
Kwa
upande wake mwandishi mkongwe na aliyetunukiwa tuzo ya maisha mwaka
2012 na Baraza la Habari Hamza Kasongo alisema vyombo vya habari vina
nguvu kubwa katika kushawishi hivyo vitumie nguvu hiyo kama muhimili wa
nne wa nchi katika kuzikabili changamoto zilizopo.
“Kuwe
na mtandao unaoeleweka wa mawasaliano kati ya waandishi wa habari
nchini ili kuhakikisha kuwa matatizo yaliyopo yanatatuliwa bila woga na
kwa ujasiri kwa lengo la kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa,” alisema
Kasongo.
0 comments:
Chapisha Maoni